Dalili za mimba changaa . | Dalili za mwanzo za mimba .

 

 Dalili za mimba changa .

Dalili za mwanzo za mimba au dalili za mimba changa ni zipi ? Dali za mimba changa hutofautina baina ya mtu mmoja na mwengine kutokana na kuwa miili huwa ina utofauti mkubwa .

Hizi ndizo dalili za mimba changa au dalili za mwanzo za mimba .

·       Kuujihisi mgonjwa asubuhi ghafla .

Hii hutokana na kuongezeka kwa hormoni nyingi za mimba kwenye damu yako kama vile Oestrogen HCG na kadhalika amabazo hukufanya ujihisi mgonjwa .

·       Kuhisi haja ndogo kila baada ya muda mfupi.

Hii hutokana na hormoni kama vile progesterone ambazo hufanya misuli kwenye utumbo na kibofu kulegea .Matokeo yake ni kuwa utajihisi haja ndogo kila baada ya muda mfupi.

·       Kukosa hedhi zako kwa wakati unaostahili.

Hedhi huashiria mwanzo katika mwezi unaofuata wa mzunguko wako .Kukosa hedhi ni dalili ya mwanzo ya mimba au dalili ya mimba changaa kutokana na kuwa ukosefu wa hedhi huashiria kuwa yai lilotengezwa lifanikiwa kukutana na mbegu za kiume na kutengeza mtoto.Hivyo basi ikiwa umekosa hedhi zako ni vyema ukatafute kipimo cha mimba ili ukapime .

·       Kuhisi kichefuchefu au kutapika .

    Kichefuchefu au kutapika ni dalili ya mwanzo ya mimba au ni dalili ya mimba changaa kutokana na kuwa mimba husababisha kuongezeka kwa homoni kwenye damu yako .Homoni hizi huifanya misuli ya tumbo lako itulie hivo basi kusababisha chakula kisagike kwa pole pole sana .Matokeo yake ni kuwa utajihisi kichefuchefu kikali haswa asubuhi unapoamka .

·       Kujihisi kiungulia kikali na kuvimbiwa na tumbo .

Kiungulia kikali na kuvimbiwa na tumbo hutokana na kuwa mimba husababisha homoni kama vile HCG ziongezeke kwenye mwili wako .Homoni hizi husababisha chakula tumboni kwako kisagike pole pole hivo basi kusababisha uhisi kiungulia kikali na kuvimbiwa .

·       Kujihisi kuchoka ghafla.

Kuhisi kuchoka ghafla ni dalili ya mimba changaa au dalili ya mwanzo ya mimba .Dalili hii hutokana na kwanza kuongezeka kwa homoni katika mwili wako na pili kutokana na kuwa mwili wako unaanza kutumia madini na nguvu nyingi kujitayarisha kutengueza mtoto.

·       Dalili nyingine ya mwanzo ya mimba changa ni kuhisi kuvurugikiwa .Hii mara nyingi husababishwa na homoni iitwayo HCG na oestrogen. Homoni hizi huhusishwa san ana dalili hii .Mara nyingi utajihisi uko na furaha na baaada ya muda mfupi utakua wajihisi kulia .

·       Kupata hedhi nyepesi sana zenye matone matone .Mara nyingi dalili hii hutokana kuwa mimba inaunganika na ukuta wa nyumba yam toto. Dalili hii huonekana katika wiki moja au mbili baada ya kujamiana .

 

Popular posts from this blog

How to file KRA Returns on ecitizen . How to file nil returns on Ecitizen

Why kipchumba murkomen - shoot to kill orders are illegal and dangerous

Pregnancy Symptoms and Signs After One Day and One Month